MENEJA wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kati Hawa Lweno,akitoa elimu kwa wananchi waliotembelea banda la EWURA katika maonesho ya Nanenane yanayoendelea katika kiwanja cha Nzuguni jijini Dodoma.
Na Alex Sonna-DODOMA
MENEJA wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) Kanda ya Kati Hawa Lweno, amesema Mamlaka hiyo imeshirikiana kikamilifu na wadau mbalimbali katika maonesho ya Nanenane kwa lengo la kutoa elimu kuhusu huduma zinazodhibitiwa na EWURA.
Timu ya wataalamu kutoka sekta za umeme, petroli,gesi asilia, maji na usafi wa mazingira , gesi pamoja na huduma kwa wateja wapo katika banda la EWURA ikitoa elimu kuhusu kazi na huduma zinazofanywa na mamlaka hiyo, ikiwemo kutoa leseni, kudhibiti ubora wa huduma na kuhakikisha upatikanaji na matumizi sahihi na salama ya huduma za nishati na maji.
Lweno amesema wadau wengi wamefika kupata elimu na kutoa maoni yao, wakiwemo wakulima, wadau wa nishati na maji, wamiliki wa vituo vya mafuta na wananchi wanaopata huduma za umeme na gesi.
Ameeleza kuwa changamoto kubwa ni upatikanaji wa mafuta vijijini, ambapo EWURA imekuwa imeweka masharti nafuu na kuendelea kutoa elimu kwa wakulima na wadau kuhusu namna ya kusogeza huduma hizo maeneo ya pembezoni jambo ambalo ameeleza kuwa limepata mwitikio mkubwa.
“Kwa mjini kituo kinaweza kuwa na mauzo ya hadi milioni 100 kwa siku na pampu nyingi, wakati vijijini kinaweza kufikia milioni 20 pekee na pampu moja tu, hivyo nitoe wito kwa watanzania hususani wakulima kuiona fursa hii” amesema.
Aidha, amesema EWURA imeendelea kuelimisha wananchi kuhusu taratibu za kupata leseni za kutoa huduma za nishati na maji, jambo ambalo limeongeza uelewa na hamasa ya wananchi wengi kutaka kufahamu zaidi.
Lweno pia amebainisha kuwa masuala ya maji yamekuwa miongoni mwa hoja zinazojitokeza zaidi katika maonesho hayo, ambapo baadhi ya wateja wameonesha wasiwasi kuhusu ubora wa maji wanayoyapata na EWURA imewahakikishia kuwa ubora wa maji ni eneo ambalo imekuwa ikilifuatilia kwa umakini.
Aidha amesema EWURA, imekuwa ikiwapa wananchi elimu kuhusu vigezo vya ubora na usalama wa maji.
Ametumia nafasi hiyo kutaka wananchi wote wanaotembelea maonesho ya Nanenane kufika katika banda la EWURA ili kupata elimu zaidi ya masuala ya udhibiti wa huduma za nishati na maji.
Thursday, August 7, 2025
EWURA YATOA ELIMU KWA UMMA KATIKA MAONESHO YA NANENANE
Tags
# Habari
Kuhusu - Singidaniblog
Habari
Tags:
Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
𝗡𝗶 𝗰𝗵𝗼𝗺𝗯𝗼 𝗰𝗵𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶 𝗸𝗶𝗻𝗮𝗰𝗵𝗼𝘁𝗼𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶 𝗻𝗮 𝗺𝗮𝘁𝘂𝗸𝗶𝗼 𝗺𝗯𝗮𝗹𝗶𝗺𝗯𝗮𝗹𝗶 𝗻𝗰𝗵𝗶𝗻𝗶 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮 𝗻𝗮 𝗸𝗼𝗸𝗼𝘁𝗲 𝗱𝘂𝗻𝗶𝗮𝗻𝗶 ,𝗸𝘄𝗮 𝗸𝘂𝗷𝗮𝗹𝗶 𝘄𝗲𝗹𝗲𝗱𝗶 𝗻𝗮 𝘁𝗮𝗮𝗹𝘂𝗺𝗮 𝘆𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶. 𝗞𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗧𝗔𝗡𝗚𝗔𝗭𝗢 𝗡𝗔 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗛𝗔𝗕𝗔𝗥𝗜, 𝗪𝗔𝗦𝗜𝗟𝗜𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔𝗦𝗜, 𝟬𝟳𝟱𝟰 𝟯𝟲𝟮 𝟵𝟵𝟬. 𝟬𝟲𝟴𝟴 𝟵𝟭𝟰 𝟯𝟰𝟰 𝗘𝗺𝗮𝗶𝗹: 𝘀𝗶𝗻𝗴𝗶𝗱𝗮𝗻𝗶𝟳𝟳@𝗴𝗺𝗮𝗶𝗹.𝗰𝗼𝗺,










No comments:
Post a Comment