𝐂𝐂𝐌, 𝐒𝐖𝐀𝐏𝐎 𝐙𝐖𝐈𝐌𝐀𝐑𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Sunday, August 16, 2026

𝐂𝐂𝐌, 𝐒𝐖𝐀𝐏𝐎 𝐙𝐖𝐈𝐌𝐀𝐑𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐔𝐒𝐇𝐈𝐑𝐈𝐊𝐈𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐊𝐈𝐇𝐈𝐒𝐓𝐎𝐑𝐈𝐀

KISIWANDUI, ZANZIBAR | 16 AGOSTI 2026

Katibu Mkuu CCM, Balozi Dkt. Asha-Rose Migiro, amempokea Katibu Mkuu SWAPO, kutoka Namibia, Ndugu Sophia Shaningwa, na kufanya naye mazungumzo katika Afisi Kuu ya CCM Kisiwandui, Zanzibar.

Mazungumzo hayo yamelenga kuimarisha zaidi uhusiano wa kihistoria kati ya CCM na SWAPO, hususan kwa kuongeza ushirikiano na mafunzo ya uongozi kwa vijana, wanawake na taasisi za vyama.

Viongozi hao pia wamejadili umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na kuendeleza mshikamano miongoni mwa vyama vya ukombozi vya Kusini mwa Afrika.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad