Kulea mtoto na kutamani kumwona akikua akiwa na maadili mema, heshima, na mwelekeo mzuri wa maisha ni ndoto ya kila mzazi.
Hata hivyo, pale mtoto wako wa kumzaa anapogeuka kuwa kero ya mtaa, anapojihusisha na wizi, uraibu wa dawa za kulevya, na tabia za kihuni, furaha yote ya uzazi hutoweka na kubaki maumivu makubwa.
Kwa zaidi ya miaka mitatu, nilipitia mateso mazito kutokana na tabia za mwanangu wa kiume. Alianza kwa kuiba vitu vidogo nyumbani kama pesa na simu, lakini baadae tabia hiyo ilikua na kuanza kuvunja nyumba za majirani na kuiba mali za watu mtaani.










No comments:
Post a Comment