𝐖𝐀𝐍𝐍𝐄 𝐖𝐀𝐏𝐀𝐍𝐃𝐈𝐊𝐈𝐙𝐖𝐀 𝐅𝐈𝐆𝐎, 𝟑𝟖 𝐖𝐀𝐅𝐀𝐍𝐘𝐈𝐖𝐀 𝐔𝐏𝐀𝐒𝐔𝐀𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈𝐏𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐔𝐉𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔 𝐌𝐍𝐇-𝐌𝐋𝐎𝐆𝐀𝐍𝐙𝐈𝐋𝐀 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, August 25, 2026

𝐖𝐀𝐍𝐍𝐄 𝐖𝐀𝐏𝐀𝐍𝐃𝐈𝐊𝐈𝐙𝐖𝐀 𝐅𝐈𝐆𝐎, 𝟑𝟖 𝐖𝐀𝐅𝐀𝐍𝐘𝐈𝐖𝐀 𝐔𝐏𝐀𝐒𝐔𝐀𝐉𝐈 𝐖𝐀 𝐌𝐈𝐒𝐇𝐈𝐏𝐀 𝐘𝐀 𝐊𝐔𝐂𝐇𝐔𝐉𝐀 𝐃𝐀𝐌𝐔 𝐌𝐍𝐇-𝐌𝐋𝐎𝐆𝐀𝐍𝐙𝐈𝐋𝐀

Hospitali ya Taifa Muhimbili–Mloganzila kwa kushirikiana na wataalam kutoka Korea Kusini, imewapandikiza figo wagonjwa wanne na wengine 38 wamefanyiwa upasuaji wa kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu katika kambi maalum iliyofanyika Agosti 15–19, 2026.

Tangu huduma hizo zianze kutolewa Muhimbili-Mloganzila mwaka 2023, jumla ya wagonjwa 28 wamepandikizwa figo na wagonjwa 289 wamefanyiwa upasuaji wa kutengeneza na kurekebisha mishipa ya kuchuja damu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dkt. Godlove Mfuko, Mkurugenzi Msaidizi wa Huduma za Upasuaji, amesema wagonjwa wote wameendelea vizuri na wameruhusiwa kwenda nyumbani.

Dkt. Mfuko amesema mafanikio hayo yameonesha matokeo ya uwekezaji mkubwa uliyofanywa na Serikali katika kuboresha miundombinu ya kutolewa huduma za afya, vifaa tiba vya kisasa pamoja na mafunzo ya wataalam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad