𝐖𝐈𝐙𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐉𝐈 𝐘𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐏𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐆𝐑𝐈𝐃𝐢 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐉𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐌𝐀𝐓𝐈 𝐘𝐀 𝐁𝐔𝐍𝐆𝐄 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, August 15, 2026

𝐖𝐈𝐙𝐀𝐑𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐉𝐈 𝐘𝐀𝐖𝐀𝐒𝐈𝐋𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐌𝐏𝐀𝐍𝐆𝐎 𝐖𝐀 𝐆𝐑𝐈𝐃𝐢 𝐘𝐀 𝐓𝐀𝐈𝐅𝐀 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐉𝐈 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐀𝐌𝐀𝐓𝐈 𝐘𝐀 𝐁𝐔𝐍𝐆𝐄

Wizara ya Maji imewasilisha taarifa ya utekelezaji wa mpango wa ujenzi wa Gridi ya Taifa ya Maji kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira.

Naibu Waziri wa Maji Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (Mb) akiwasilisha taarifa hiyo kwa niaba ya Waziri wa Maji amesema utekelezaji huo ulishaanza kwa kutekeleza miradi mikubwa ya maji ambayo inatumia vyanzo vya uhakika vya Maji ikiwemo mradi wa maji ya ziwa Victoria ambayo yamefika Shinyanga hadi wilaya za mkoa wa Tabora na kazi ikiendelea kufikisha maji Dodoma.

Amesema Gridi ya Taifa ya Maji ambayo ni kichocheo kikubwa cha kufikia malengo ya Dira ya Maendeleo ya 2050 unatarajiwa kuwa na mtandao wenye urefu wa zaidi ya Km 6200 ambao utahusisha mitaro ya wazi zaidi ya Km 1200 na mabomba zaidi ya Km 5000.

Mradi huo utatekelezwa kwa awamu tatu hadi kukamilika kwake mwaka 2050.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) amepongeza na kutaka uzingatiaji wa mahitaji yote ya maji kwa matumizi ya nyumbani, mifugo na mimea.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad