Na Mwandishi
Wetu, Tanga
SERIKALI kupitia
Wizara ya Elimu, Sayansi na Tekinolojiia imetoa zaidi ya shilingi Bilioni 156
katika Mkoa waTanga kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya kujifunza na
kufundishia.
Hayo
yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk. Batilda Salha Burian, alipokuwa
akizungumza na Waandishi wa habari kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya Maonesho
ya Wiki ya Taifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, yanayofanyika katika Viwanja
vya Usagara, Jijini Tanga.
Alisema
mgeni rasmi wa ufunguzi wa Maonesho hayo ni Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda Agosti 18, 2026.
Alisema maonesho hayo ni jukwaa muhimu linalotoa fursa kwa Tanzania kuweza kujipima kimataifa, huku likionesha mwelekeo wa nchi katika sekta za ufundi, ubunifu na utafiti.
“ Katika
Maonesho haya zaidi ya taasisi 300 zimejitokeza kushiriki huku zikiwasilisha
bunifu, tafiti na teknolojia zinazoendana na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia
duniani,” alisema Burian.
Alizitaja taasisi
hizo kuwa ni vyuo vikuu mbalimbali nchini, taasisi za utafiti wa kisayansi na
kiufundi, vyuo vya ufundi stadi na vya kati, pamoja na taasisi binafsi
zinazojihusisha na masuala ya sayansi, teknolojia na ubunifu.
Balozi Dkt.
Burian amewataka wananchi, wataalamu, wanafunzi na wadau wa elimu kujitokeza
kwa wingi kushuhudia bunifu mbalimbali na kujifunza teknolojia mpya
inazochagiza maendeleo ya kiuchumi na kijamii hapa nchini.
Kwa upande
wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu na Ufundi stadi (NACTIVET)
Mwajuma Lingwanda amesema Baraza hilo limeandaa mashindano ya ujuzi Kitaifa
mwaka 2026.









No comments:
Post a Comment