Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wanachama wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika (AU-PSC) kujadili hali ya usalama nchini Libya.
Mkutano huo umeongozwa na Rais wa Jamhuri ya Uganda na Mwenyekiti wa Baraza hilo, Mheshimiwa Yoweri Kaguta Museveni, leo tarehe 24 Julai, 2025 kwa njia ya mtandao ambapo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni miongoni wa nchi mwanachama wa Baraza hilo ambalo linaundwa na nchi 15 za Umoja wa Afrika.
Katika Mkutano huo, Bashungwa kwa niaba ya Rais Samia amepongeza Juhudi za Mheshimiwa Denis Sassou Nguesso, Rais wa Jamhuri ya Congo na Mwenyekiti wa AU High Level Committee on Libya, hususani kwa kusimamia The National Reconcilliation Charter ambayo inatoa muongozo wa suluhu ya mgogoro nchini Libya ikiwemo kufanyika kwa uchaguzi, kuimarisha taasisi nchini Libya hususan Jeshi.
Thursday, July 24, 2025
Home
Habari
BASHUNGWA AMWAKILISHA RAIS SAMIA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI KUJADILI HALI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA NCHINI LIBYA
BASHUNGWA AMWAKILISHA RAIS SAMIA MKUTANO WA WAKUU WA NCHI KUJADILI HALI YA SIASA, ULINZI NA USALAMA NCHINI LIBYA
Tags
# Habari
Kuhusu - Singidaniblog
Habari
Tags:
Habari
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
𝗡𝗶 𝗰𝗵𝗼𝗺𝗯𝗼 𝗰𝗵𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶 𝗸𝗶𝗻𝗮𝗰𝗵𝗼𝘁𝗼𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶 𝗻𝗮 𝗺𝗮𝘁𝘂𝗸𝗶𝗼 𝗺𝗯𝗮𝗹𝗶𝗺𝗯𝗮𝗹𝗶 𝗻𝗰𝗵𝗶𝗻𝗶 𝗧𝗮𝗻𝘇𝗮𝗻𝗶𝗮 𝗻𝗮 𝗸𝗼𝗸𝗼𝘁𝗲 𝗱𝘂𝗻𝗶𝗮𝗻𝗶 ,𝗸𝘄𝗮 𝗸𝘂𝗷𝗮𝗹𝗶 𝘄𝗲𝗹𝗲𝗱𝗶 𝗻𝗮 𝘁𝗮𝗮𝗹𝘂𝗺𝗮 𝘆𝗮 𝗵𝗮𝗯𝗮𝗿𝗶. 𝗞𝗪𝗔 𝗠𝗔𝗧𝗔𝗡𝗚𝗔𝗭𝗢 𝗡𝗔 𝗛𝗨𝗗𝗨𝗠𝗔 𝗬𝗔 𝗛𝗔𝗕𝗔𝗥𝗜, 𝗪𝗔𝗦𝗜𝗟𝗜𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔𝗦𝗜, 𝟬𝟳𝟱𝟰 𝟯𝟲𝟮 𝟵𝟵𝟬. 𝟬𝟲𝟴𝟴 𝟵𝟭𝟰 𝟯𝟰𝟰 𝗘𝗺𝗮𝗶𝗹: 𝘀𝗶𝗻𝗴𝗶𝗱𝗮𝗻𝗶𝟳𝟳@𝗴𝗺𝗮𝗶𝗹.𝗰𝗼𝗺,











No comments:
Post a Comment