Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam
MFANYABIASHARA na Mshindi wa kura za maoni katika kinyang’anyiro cha ubunge Jimbo la Ilongero mkoani Singida Haider Gulamali aliamsha shangwe wakati wa Harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwaka huu iliyofanywa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ikiongozwa na Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima
Dendegu ambaye alikuwa na dharura na kushindwa kuhudhuria kwenye harambee hiyo
iliyofanyika Agosti 12, 2025 Ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar es Salaam Gulamali alianza kwa kumpongeza Rais Samia na kuimba
wimbo maarufu unaoimbwa na wana CCM wa wembe ni uleule ushindi.
Gulamali alihoji wembe huo unatoka wapi na kueleza umetoka
kwenye saluni ya CCM na wote waliokuwa wanauimba wamenyolewa na
watakuja kuuona tena baada ya miaka mitano ‘akimaanisha waalikwa wote waliohudhuria na kuchangia harambee hiyo.
Akizungumza wakati akichangia harambee hiyo alisema Kampuni ya Africarriers Sh.
Milioni 50. Sajjad Haider Sh. Milioni 25 na mengine Gulamali Group and Associates Sh. Milioni 125 na mengine kwa pamoja jumla kuu ikiwa ni Sh. Milioni 300.
Katika harambee Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan alichangia Sh.
Milioni 100.
Katibu Mkuu wa chama hicho Dkt. Emmanuel
Nchimbi akizungumza na wahariri na waandishi wa habari jijini hapa Agosti 11,
2025 alisema harambee hiyo inalenga
kukusanya Shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya maandalizi ya kampeni, ikiwemo
gharama za magari, mafuta, fulana, mabango, kanga na mambo mengine.
Ndugu Haider Gulamali akiwa katika picha tofauti wakati wa harambee hiyo.









No comments:
Post a Comment