WAKILI MADELEKA AIBUKA KIDEDEA KURA ZA MAONI JIMBO LA KIVULE ACHUKUA FOMU ZA UBUNGE - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Friday, August 15, 2025

WAKILI MADELEKA AIBUKA KIDEDEA KURA ZA MAONI JIMBO LA KIVULE ACHUKUA FOMU ZA UBUNGE

Wakili Peter Madeleka akionesha begi lenye fomu za kugombea Ubunge Jimbo la Kivule lililopo Ilala Jijini Dar es Salaam baada ya kukabidhiwa.

.............................................. 

Mwandishi Wetu

WAKILI Peter Madeleka, ameibuka na ushindi katika kura za maoni kuwania kupitishwa na Chama cha ACT Wazalendo kugombea Jimbo la Kivule.

Iwapo kamati Kuu ya ACT Wazalendo itampitisha atakuwa mgombea wa Jimbo hilo kupitia Chama hicho katika uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika mwezi Oktoba, mwaka huu.

Katika uchaguzi huo uliofanyika mapema wiki hii, Wakili Madeleka alishinda kwa kupata kura 38 huku mpinzani wake Colman Marwa akipata kura 12. Hata hivyo, Marwa atagombea udiwani kata ya Kitunda moja ya kata Sita za Jimbo hilo.

Akitangaza matokeo hayo msimamizi wa uchaguzi huo, Risasi Semasaba, alimtangaza pia Nice Marwa kuwa mgombea Ubunge Viti Maalum Jimbo hilo na mgombea udiwani kata ya Msongola.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi, Wakili Madeleka aliwashukuru wapiga kura kwa kumwamini, akizidi kuwaomba waendelee kumwunga mkono katika safari nzima kwa kuwa huo ni mwanzo tu.

Kwa upande wake Marwa baada ya kupewa fursa ya kuzungumza alisema “Ndugu wajumbe nashukuru sana kwa kura mlizonipa, naomba sasa tuwe pamoja tumwunge mkono Bw. Madeleka.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad