Siku ambayo ndugu yangu alitoweka ni siku ambayo sitawahi kuisahau maishani mwangu. Tulikuwa familia ya karibu sana.
Ingawa kila mmoja alikuwa na maisha yake, tulikuwa tunawasiliana mara kwa mara. Ndugu yangu alikuwa mtu wa kupenda familia, mchangamfu, na hakuwa mtu wa kukaa kimya kwa muda mrefu bila kutoa taarifa.
Ndiyo maana kila kitu kilipoanza, hakuna aliyedhani kingekuwa kikubwa vile. Mwanzoni tuliona kama jambo la kawaida. Kulikuwa na siku simu yake haikupatikana. Tulidhani labda alikuwa busy au alisafiri ghafla. Lakini siku zilipoanza kupita bila message wala simu yoyote, moyo wangu ulianza kupata wasiwasi.










No comments:
Post a Comment