𝗪𝗔𝗡𝗔𝗥𝗨𝗗𝗜 𝗡𝗬𝗨𝗠𝗕𝗔𝗡𝗜 𝗖𝗛𝗜𝗠𝗕𝗨𝗞𝗢 𝗟𝗔 𝗔𝗦𝗜𝗟𝗜 𝗬𝗔𝗢 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, May 25, 2026

𝗪𝗔𝗡𝗔𝗥𝗨𝗗𝗜 𝗡𝗬𝗨𝗠𝗕𝗔𝗡𝗜 𝗖𝗛𝗜𝗠𝗕𝗨𝗞𝗢 𝗟𝗔 𝗔𝗦𝗜𝗟𝗜 𝗬𝗔𝗢

 Mwandishi Wetu,

Kumekuwa na mwitikio mkubwa wa watalii wa ndani kutembelea hifadhi ya Ngorongoro hii ikimaanisha wanarudi nyumbani eneo ambalo ndilo pekee lenye ushahidi wa kisayansi usiotiliwa shaka kuwa ndio chanzo cha binadamu wa kale.

Safari hii ni zamu ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT ) chini ya Mchungaji Kiongozi wa Kanisa  hilo Usharika wa Kijitonyama jijini Dar es Salaam Rev, Dr. Elliona Kimaro aliyeongoza kundi la wanaume 300 kutoka mikoa mbalimbali nchini kutembea Makumbusho ya Jiopaki ya Ngorongoro-Lengai (Urithi Geopark) na vituo vya hifadhi vilivyopo Ngorongoro 

Akiwa na Ujumbe huo Dkt.  Kimaro amesema makundi mbalimbali kuhamasika kufanya utalii wa Ndani wanavutiwa na vitu mbalimbali ikiwemo kushuhudia uumbaji wa Mungu, kuona na kujifunza Chanzo cha asili ya Mwanadamu katika bonde la Olduvai na Laetoli, kuona Ikolojia ya hifadhi pamoja na utunzaji wa Mazingira kama vitabu vitakatifu vinavyohimiza.

"Tumekuja Nyumbani Ngorongoro kwenye asili ya Mwanadamu tukiwa na kundi la wanaume 300,  tumeshuhudia uumbaji wa Mungu, utunzaji wa Ikolojia, Mazingira, Misitu Wanyama wa kila aina ya vyote vilivyoumbwa kwa mfano wa Mungu" alisema  Dkt. Kimaro.

Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inawarudisha nyumbani binadamu wote ili kushuhudia asili yao ambapo binadamu alianza kutembea na kufanya shughuli zake kwa miguu miwili.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad