𝗕𝗢𝗡𝗗𝗜𝗔 𝗠𝗠𝗔𝗥𝗘𝗞𝗔𝗡𝗜 𝗔𝗙𝗨𝗥𝗔𝗛𝗜𝗔 𝗠𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗭𝗜 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔, 𝗔𝗝𝗜𝗔𝗡𝗗𝗔𝗔 𝗞𝗨𝗢𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗝𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 𝗦𝗘𝗥𝗘𝗡𝗚𝗘𝗧𝗜 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Monday, May 25, 2026

𝗕𝗢𝗡𝗗𝗜𝗔 𝗠𝗠𝗔𝗥𝗘𝗞𝗔𝗡𝗜 𝗔𝗙𝗨𝗥𝗔𝗛𝗜𝗔 𝗠𝗔𝗣𝗢𝗞𝗘𝗭𝗜 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔, 𝗔𝗝𝗜𝗔𝗡𝗗𝗔𝗔 𝗞𝗨𝗢𝗡𝗔 𝗠𝗔𝗔𝗝𝗔𝗕𝗨 𝗬𝗔 𝗦𝗘𝗥𝗘𝗡𝗚𝗘𝗧𝗜

Bondia wa kimataifa wa Marekani Terence “Bud” Crawford amesifu ukarimu wa Watanzania tangu alipowasili nchini Mei 24, 2026, kwa ziara ya kitalii.


Bondia huyo ameyasema hayo alipokutana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi jijini Dar es Salaam akianza ziara yake ya siku kadhaa nchini.

Bondia huyo mwenye rekodi ya kutopoteza pambano lolote katika michezo 42 aliyocheza tangu aingie ndondi za kulipwa, ameeleza pia kusubiri kwa hamu kuona maajabu ya vivutio kama Serengeti, Ngorongoro na Zanzibar atakakotembelea.

Kwa upande wake Dkt. Abbasi kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amemkaribisha nchini na kumwalika kuendelea kuja Tanzania kila atakapohitaji hasa wakati huu ambapo ameamua kustaafu mapema mchezo huo tangu Disemba mwaka jana 2025.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad