Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua program ya mafunzo ya Uzamili ya Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida ambayo kwa mara ya kwanza imetoa Wahitimu wa Shahada ya Uzamili katika mahafali ya kihistoria yaliyofanyika Juni 5, 2026...............................
TAASISI ya
Uhasibu Tanzania (TIA) Kampasi ya Singida kwa mara ya kwanza imetoa Wahitimu wa Shahada ya Uzamili katika mahafali ya kihistoria.
Katika
Mahafali hayo ya 24 wahitimu
548 kutoka Kampasi za Dar es Salaam, Zanzibar, Mtwara, Kigoma na Singida
wametunukiwa Shahada za Uzamili.
Mkuu wa Mkoa
wa Singida, Halima Dendego ambaye alikuwa mgeni rasmi akifungua program ya
mafunzo ya uzamili Juni 5, 2026 alisema mahafali hayo ni hatua muhimu kwa mkoa
wa Singida katika kuendelea kuzalisha wataalamu bobezi wanaohitajika katika
sekta mbalimbali za umma na sekta binafsi.
“Wakati
tunaianza hii safari na mimi nilikuwemo hivyo ni sehemu ya mafanio haya
ambayo yametoa fursa kwa wana Singida hasa watumishi wa umma kuweza
kujiendeleza na leo tunaona ushuhuda wa watumishi waliotoka maeneo mbalimbali
katika mkoa wetu wa Singida,” alisema Dendego.
Dendego
aliwaambia wahitimu hao kuwa mafanikio hayo wanayosherehekea ni ya kitaaluma
ambayo yametokana na bidii, juhudi, nidhamu, uvumilivu na kujituma kwao katika
kutafuta elimu.
Alisema kwa
kufanya hivyo wametimiza maamurisho ya Mwenyezi Mungu ambaye amesema kwenye
vitabu vyote vya dini kuwa wsimuache elimu akaenda zake na waaende popote pale
hata uchina hivyo wametekeleza maagizo hayo.
Aidha,
alisema wametekeleza mapendekezo na malengo ya Serikali nay a familia zao hivyo
anawapongeza kwa hatua hiyo ambayo wameifikia na kuwa siyo mwisho wanahitaji
kusonga mbele hadi wafike juu kabisa.
Dendego
aliwaambia wahitimu hao kuwa kila kizazi hupewa jukumu lake na jukumu la kizazi
chao ni kuhakikisha Tanzania inanufaika na mapinduzi ya teknolojia, maarifa na
ubunifu unaoendelea kote duniani kwa kuleta tija, ushindani na fursa ya maendeleo
ya haraka kwa ajili ya kuendeleza maendeleo ya wananchi, jamii na Taifa kwa
ujumla.
“Naamini elimu mliyopata imewafanya kujitambua nan i tegemeo la taifa lisiloona mdudu rushwa nendeni mkakae mbali na mambo haya, mkatusaidie kuyapiga vita ili tuwe na jamii salama wakati wote, inaumiza sana kuona muhitimu wa levo yenu anaenda kuipeleka kwenye uraibu, kupelekwa kwenye vyombo vya dola kwa sababu ya rushwa na amini haya yote mmesisitizwa na taifa linawategemea,” alisema Dendego.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Profesa William Pallangyo
akitoa taarifa kwenye mahafali hayo alisema katika mahafali hayo ya 24 Wahitimu
548 wametunukiwa shahadi hiyo kutoka Kampasi za Dar es Salaam, Zanzibar,
Mtwara, Kigoma na Singida.
Alisema kati
ya wahitimu hao, wanawake ni 264 sawa na asilimia 48, na wanaume ni 284 sawa na
asilimia 52.
Alisema Jumla
ya wahitimu 177 wa kampasi za Dar es Salaam, Zanzibar, na Singida, wametunukiwa
Shahada ya Uzamili. Kati ya hao, wanawake ni 56 sawa na asilimia 32 na wanaume
ni 121 sawa na asilimia 68.
Alisema Wahitimu
wengine 371 kutoka kampasi za Dar es Salaam, Mtwara na Kigoma, wametunukiwa Cheti
cha Awali, Astashahada na Stashahada.
“Nawapongeza wahitimu wote kwa juhudi, nidhamu na uvumilivu walioonesha hadi kufikia hatua hii muhimu katika maisha ya kitaaluma,” alisema Profesa Pallangyo.
Akizungumzia mafanikio ya Kampasi ya Singida alisema Taasisi imeendelea kupiga hatua kubwa katika utekelezaji wa majukumu yake ya msingi sambamba na uboreshaji wa miundombinu ya kufundishia na kujifunzia.
Profesa Pallangyo alisema mafanikio hayo yanatekelezwa kupitia ufadhili wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Rais Dkt. Samiaa Suluhu Hassan kupitia Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Vyuo vya Elimu ya Juu (HEET) kwa usimamizi wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Miongoni mwa mafanikio yaliyopatikana ni u jenzi wa Jengo la Taaluma katika Kampasi ya Singida ambalo limegharimu Shilingi bilioni 13.5 ambao ujenzi wake umefikia asilimia 60.
Aidha, aliongeza kuwa Kampasi ya Mwanza kuna ujenzi wa hosteli mbili za wanafunzi ambapo ujenzi wake umegharimu Shilingi bilioni 7.2 na umefikia asilimia 95 ya utekelezaji.
Alisema Taasisi ya Uhasibu Tanzania ina miradi mingine ya ujenzi wa Majengo ya taaluma na utawala katika Kampasi ya Kigoma ambayo inagharimu Shilingi bilioni 11.08 na yamekamilika kwa asilimia 98.
Akizungumzia ujenzi wa majengo ya taaluma, utawala na mabweni katika Kampasi ya Zanzibar ambayo yamegharimu Shilingi bilioni 15.9 alisema ujenzi wake umefikia asilimia 30 ya utekelezaji.
Kukamilika kwa
miundombinu hiyo, kutaiwezesha Taasisi hiyo kuongeza udahili sambamba na ubora wa
huduma za mafunzo.
Alisema kwa mwaka 2025/2026 Taasisi hiyo imefanya zaidi ya tafiti 13 na kuzalisha machapisho 60 ya kitaaluma katika maeneo mbalimbali.
Profesa Pallangyo aliongeza kuwa Watumishi
24 wanaendelea na masomo ya Shahada ya Uzamivu (PhD) katika vyuo mbalimbali
nchini na nje ya nchi.
Kwa upande
wake Mjumbe wa Bodi Renetus Msangira akimwakilisha Mwenyekiti wa Bodi ya
Ushauri ya Wizara alisema kuhitimishwa kwa kundi la kwanza la Shahada ya
Uzamili katika Kampasi ya Singida ni hatua muhimu katika kuongeza fursa za
elimu ya juu nchini.
Alisema Bodi
ya Ushauri ya Wizara, itaendelea kusimamia na kuunga mkono juhudi za
kuhakikisha Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) inabaki kuwa taasisi ya mfano
katika utoaji wa elimu, utafiti na ushauri wa kitaalam.
Msangira
alitumia nafasi hiyo kutoa shukukrani kwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya
uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
katika kuendelea kuimarisha sekta ya elimu ya juu nchini kupitia uwekezaji
katika miundombinu, rasilimali watu, Mifumo ya TEHAMA na mazingira bora ya
kujifunzia katika Taasisi hiyo ya Uhasibu Tanzania.
Akitoa
nasaha kwa Wahitimu Msangira alisema elimu waliyopata ni zaidi ya cheti au
shahada.
“Elimu mliyopata ni dhamana ya kutumia maarifa, ujuzi na weledi wenu, kuleta mabadiliko chanya katika jamii,” alisema Msangira.
Imeandaliwa na Mtandao wa singidaniblog.co.tz
Simu namba: 0754 362990 / 0688 914 344
👇TAZAMA VIDEO HAPA CHINI
Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Profesa William Pallangyo akitoa taarifa kwenye mahafali hayo.
Mjumbe wa Bodi Renetus Msangira kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara, akizungumza.
Mshereheshaji (MC) wa mahafali hayo, Imani Matonya akiwajibika.
Mkurugenzi wa TIA Kampasi ya Singida Dkt. James Mrema, akizungumza.
Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo
Mahafali yakiendelea
Ndugu ,Jamaa, Marafiki na Wazazi wa Wahitimu wakiwa kwenye mahafali hayo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego ambaye alikuwa mgeni rasmi akiwa na viongozi wengine meza kuu. Kulia ni Prof. Momole Kasambala, Makamu Mkuu wa Chuo - Taaluma, Utafiti na Ushauri na Mkurugenzi wa TIA Kampasi ya Singida, Dkt. James Mrema.
Mahafali yakiendelea
Wahadhiri wakiwa kwenye mahafali hayo
Mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego akiagana na viongozi mbalimbali.
.jpeg)
Wafanyakazi wa TIA Kampasi ya Singida wakiwa katika ubora wao kwenye mahafali hayo.
Picha ya Pamoja









No comments:
Post a Comment