𝐖𝐀𝐓𝐔𝐏𝐖𝐀 𝐉𝐄𝐋𝐀 𝐌𝐀𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐒𝐀 𝐋𝐀 𝐁𝐈𝐀𝐒𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐙𝐀 𝐃𝐀𝐖𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐄𝐕𝐘𝐀 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, June 2, 2026

𝐖𝐀𝐓𝐔𝐏𝐖𝐀 𝐉𝐄𝐋𝐀 𝐌𝐀𝐈𝐒𝐇𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐊𝐎𝐒𝐀 𝐋𝐀 𝐁𝐈𝐀𝐒𝐇𝐀𝐑𝐀 𝐙𝐀 𝐃𝐀𝐖𝐀 𝐙𝐀 𝐊𝐔𝐋𝐄𝐕𝐘𝐀

Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, imewahukumu kifungo cha maisha jela Suleiman Thabit Ngulangwa na Farid Hamis Said baada ya kutiwa hatiani kwa kosa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya heroin yenye uzito wa kilo 15.19.

Katika hukumu iliyotolewa Juni 1, 2026, Jaji S.E. Kisanya alisema ushahidi wa upande wa mashtaka ulithibitisha pasipo shaka kuwa washtakiwa hao walikuwa na umiliki wa dawa hizo.

Mchambuzi wa Serikali kutoka Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Leonida Daniel Michael, aliithibitishia mahakama kuwa pakiti 16 zilizokamatwa zilikuwa na heroin yenye uzito wa kilo 15.19 baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kisayansi.

Mahakama ilibaini kuwa utetezi wa washtakiwa haukuweza kuibua shaka dhidi ya ushahidi wa mashahidi na vielelezo vilivyowasilishwa.

Mshtakiwa wa pili, Sharifa Selemani Bakari, aliachiliwa huru baada ya mahakama kubaini kuwa upande wa mashtaka haukuthibitisha ushiriki wake katika kosa hilo.

Mbali na kifungo hicho, mahakama imeagiza heroin yote iliyokamatwa pamoja na vifaa vya kufungashia kuteketezwa kwa mujibu wa sheria.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad