...............................
MKUU wa
Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda amekabidhi rasmi jengo la Ofisi ya Shirika la
Umeme Tanzania (TANESCO) wilaya hiyo mkoani Singida baada ya ujenzi wake
kukamilika.
Ujenzi wa jengo
hilo lililojengwa na shirika hilo umegharimu Shilingi Milioni 285 na ujenzi wa
mradi huo ulianza Novemba 28, 2025.
Akizungumza Julai 4, 2026 kabla ya kukabidhi jengo hilo
Mwenda aliipongeza Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kwa maboresho makubwa ya miundombinu ya umeme
hasa ujenzi wa Bwawa la Mwalimu Nyerere.
Alisema siyo
nchi nyingi katika Bara la Afrika na hata nje ya Afrika ambazo zimefika ilipofika
Tanzania kwenye suala zima la uzalishaji na usambazaji umeme ni mafanikio
makubwa.
Mwenda alisema
miaka 30, 20 na 15 iliyopita hali ya hupatikanaji wa umeme ilikuwa ni
kizungumkuti na kukaa wiki bila ya kupata umeme ilikuwa jambo la kawaida.
“Kwa wiki ilikuwa tunapata umeme kwa siku tatu tu tena usiku lakini leo hii katika nchi yetu haiwezi ikapita siku nzima bila ya umeme kukosekana kuwaka sasa ni miaka minne na hiyo yote ni kwa sababu ya maboresho yaliyofanyika,” alisema Mwenda.
Alisema
Tanesco ilikuwa na madeni makubwa ambayo ilikuwa mzigo kwa Serikali na kwa
shirika lenyewe leo hii kwa sehemu kubwa madeni hayo yamepunguzwa kwa kiwango
kikubwa.
Mwenda
alisema hali hiyo ilitokakana na kukodi mitambo na kukunua umeme uliozalishwa
na matumizi ya mitambo iliyokuwa ikitumia dizeli kwa gharama kubwa.
“Leo tunazalisha umeme wenyewe baada ya kujenga Bwawa la Mwalimu Nyerere kwa fedha zetu wenyewe kutokana na maamuzi magumu aliyoyafanya Rais wa Tano wa nchi yetu Hayati Dk. John Pombe Magufuli ili ni jambo la kujipongeza,” alisema Mwenda.
Aidha,
Mwenda alisema Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya miaka mitano iliyopita
imeeleza kuwa tayari Tanzania imesambaza umeme kwa asilimia 51 na imebaki
asilimia 49 kwenye vitongoji na kuwa kwenye miji, mitaa na vijiji vyote vina umeme
na vimebakia vitongoji 31, 320 kwa nchi nzima.
Alisema kwa
Wilaya Iramba walikuwa na vitongoji 243 ambavyo vilikuwa na umeme kati ya
vitongoji 393, vitongoji zaidi ya 150 havikuwa na umeme mpaka mwaka jana lakini
kutokana na mpango mzuri wa Serikali tayari amepatikana mkandarasi kwa ajili ya
kuweka umeme kwenye vitongji 50.
Mwenda
aliongeza kuwa pia kuna mkandarasi mwingine anaendelea kuunganisha umeme kwenye
vitongji 18 ambapo ameeleza kuwa ndani ya miaka mitatu wilaya hiyo vitongoji
vyote vitakuwa na umeme.
Kwa upande wake Meneja wa shirika hilo Mkoa wa Singida, Mhandisi Mwamvita Ally alimshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha fedha za ujenzi wa jengo hilo la ofisi ya wilaya ambalo linakwenda kuboresha mazingira ya Wafanyakazi waweze kuifanya kwa ubora na Wananchi waweze kuhudumiwa kwenye ofisi yenye hadhi.
Aidha,
Mwamvita aliipongeza timu iyofanikisha ujenzi wa jengo hilo ambayo aliiongoza
na kufanikisha kumaliza ujenzi wake ndani ya miezi sita.
Akitoa
taarifa ya ujenzi wa mradi huo Meneja wa shirika hilo Wilaya ya Iramba,
Idefonce Arthur alisema ujenzi wa mradi huo ulianza kwa kazi ya kung’oa visiki
na kusafisha eneo la ujenzi huku mpango kaziukiwa likamilike Juni 30, 2026.
Alisema jengo
hilo lina ofisi ya Wafanyakazi, Huduma kwa Wateja pamoja na Ukumbi wa mikutano na Mitambo ya TEHAMA na kuwa mradi
huo umefikia asilimia 98 ya utekelezaji.
Akizungumzia manufaa ya mraadi huo alisema utaboresha mazingira ya kazi kwa Watumishi na kuongeza ufanisi wa huduma na kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa Wananchi wa Wilaya ya Iramba.
Alisema pia
ofisi hiyo itatumika kama kichocheo cha kuwasaidia na kuhamasisha wananchi
kutumia njia mbadala kama hatua ya kukabiliana matumizi ya kuni na mkaa kwa
maendeleo endelevu.
Arthur
alisema ofisi hiyo itasaidia kupunguza gharama kwa shirika kwa kuokoa kodi ya
kupanga jengo na usumbufu kwa wateja pale eneo la ofisi linapobadilika mara kwa
mara.
Aliongeza
kuwa ujenzi wa mradi huo ulisaaidia kutoa ajira kwa wananchi wa maeneo ya
Kiomboi na kuwa mpango wa baadaye ni kuhakikisha jengo hilo linakuwa kitovu cha
kutoa huduma bora, utawala bora na ufanisi wa Taasisi kwa muda wote kuboresha
kwa kuweka fenicha na ujenzi wa uzio.
Meneja huyo
alitumia nafasi hiyo kumshukuru Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
na Mbunge wa Jimbo la Iramba Magharibi, Dk. Mwigulu Mchemba kwa utekelezaji wa
ilani ya CCM kwa vitendo.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, akizungumza wakati wa kukabidhi ofisi hiyo. Kulia ni Meneja wa TANESCO Mkoa wa Singida Mhandisi Mwamvita Ally.
Mkuu wa Wilaya ya Iramba, Suleiman Mwenda, akikata keki maalumu wakati akikabidhi jengo hilo.
Meneja wa TANESCO Mkoa wa Singida Mhandisi Mwamvita Ally akizungumza.
Meneja wa shirika hilo Wilaya ya Iramba, Idefonce Arthur, akitoa taarifa yaa ujenzi wa jengo hilo.
Wafanyakazi wa shirika hilo wakiwa kwenye hafla hiyo.
Hafla ikiendelea.
Hafla ikiendelea.
Muonekano wa keki maalumu ya kukabidhi jengo hilo.
Muonekano wa jengo la ofisi hiyo.
Picha ya pamoja
......................................
Taarifa hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale simu namba 0754362990










No comments:
Post a Comment