PROFESA MKENDA: RAIS SAMIA NI MTU WA VITENDO KULIKO MANENO - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, August 18, 2026

PROFESA MKENDA: RAIS SAMIA NI MTU WA VITENDO KULIKO MANENO

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolph Mkenda (wa pili kulia), akipata maelezo kutoka kwa Mwanafunzi Jackline Habibu Ndee (kushoto), ambaye anajifunza masomo Amali alipotembelea banda la shule za Sekondari kabla ya kufungua Maonesho ya Wiki ya Taifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara, Jijini Tanga Agosti 18, 2026.

.............................

Na Dotto Mwaibale, Tanga


WAZIRI wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolph Mkenda amesema Rais wa Jamhuri ya Muungamo wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassani ni kiongozi wa vitendo na siyo maneno.


Profesa Mkenda ameyasema hayo wakati akifungua Maonesho ya Wiki ya Taifa ya Elimu, Ujuzi na Ubunifu 2026, yanayofanyika katika Viwanja vya Usagara, Jijini Tanga Agosti 18, 2026.


“Rais Samia katika kuendeleza maendeleo utaona kazi kubwa aliyoifanya ya kasi ya Teknolojia nchini kufikia kwenye muelekeo mzuri wa kutuwezesha kufanya shughuli zetu wenyewe badala ya kutegemea wataalamu kutoka nje,” alisema Profesa Mkenda.


Alisema kwa maelekezo ya Rais Samia hakuna haja tena ya wageni kufanya kazi kwa gharama kubwa bali zitafanywa na Watanzania.


Profesa Mkenda aliongeza kuwa katika kukamilisha jambo hilo aliagiza zijengwe sekondari za wasichana  kwa ajili ya masomo ya sayansi kila mkoa ambapo baadhi zilizokamilika tayari amezizindua.


Profesa Mkenda alisema lengo la Rais ni kuhakikisha tunaongeza uwezo wa kisayansi  kwa wanafunzi na pili kupewa nafasi ya kwenda kusoma nje ya nchi.


“ Rais Samia aliagiza kuwa ili kuwavutia wanafunzi wenye uwezo na vipaji vikubwa kusoma sayansi, hisibati, Tehama, Uhandisi na elimu tiba watapata ufadhili wa Serikali kwa asilimia 100,” alisema Profesa Mkenda.


Alisema serikali inatoa ufadhili huo kwa wanafunzi waliofanya vizuri kidato cha sita ambapo watapewa fedha za kujikimu, kulipia ada, vifaa vya shule mpaka watakapo maliza masomo yao kupitia utaratibu uliowekwa.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Carolyne Nombo, akizungumza wakati wa ufunguaji wa Maonesho hayo.Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye ufunguzi wa Maonesho hayo

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad