Kauli hiyo imetolewa na Meneja Mkazi wa Barrick Gold Mine Tanzania Melkiory Ngido wakati wa kikao baina ya Uongozi wa Kampuni hiyo na Kamishna Mkuu wa TRA Yusuph Juma Mwenda katika ofisi za TRA jijini Dar es Salaam.
Ngido amesema utaratibu uliowekwa na TRA wa kufungua milango na kukutana na Walipakodi kujadili masuala mbalimbali ya kikodi umekuwa na tija katika kuongeza uelewa wa kodi na kuhamasisha ulipaji wa kodi kwa hiari.
"Sisi tumekuwa na utaratibu wa kila mwaka kukutana na Uongozi wa TRA kueleza hali yetu ya kibiashara na namna tutakavyolipa kodi, na kama ambavyo imekuwa kwa vipindi vingine hali yetu kibiashara ni nzuri na tutaendelea kulipa kodi kwa hiari" amesema Ngido.
Kwa upande wake Kamishna Mkuu wa TRA Yusuph Juma Mwenda amesema Mamlaka hiyo itaendelea kuboresha huduma zake kwa walipakodi, kutoa elimu ya kodi na kuwezesha biashara.
Amesema TRA inatambua na kuthamini mchango wa Kodi wa Barrick Gold Mine wakiwa ni walipakodi wakubwa pamoja na walipakodi wengine kote nchini na kuwa milango ya taasisi hiyo ya Umma ipo wazi kwaajili ya kuwasikiliza na kutatua changamoto zinazowakabili walipakodi kote nchini.












No comments:
Post a Comment