................................................
Na Dotto Mwaibale, Tanga
UPENDO ni hali ya moyo wa mtu kuwa na hisia kali ya kujali, kuhurumia kuwa na uchungu dhidi ya mtu mwingine bila ya kinyongo.
Ni sifa ya
thamani inayohusisha ustahimilivu na
kutafuta mema kwa wengine kama vitabu vitakatifu vya dini zote kwa Waislaamu Qur-an
na Biblia kwa Wakristo vinavyoeleza upendo kama amri kuu, ikimaanisha ni msingi
wa maisha ya kiroho.
Mkurugenzi
Mkuu Wa Kampuni Ya GBP ya Jijini Tanga, Badar Sood ni kiongozi mwenye upendo ambaye anagusa
maisha ya watu mbalimbali.
Wananchi wa Mkoa wa Tanga na maeneo mengine ya nchi wana ujua ubinadamu wake.
Badar Sood wakati wote amekuwa mstari wa mbele
kushirikiana na wananchi katika mambo mbalimbali ya maendeleo, furaha na
huzuni.
Jambo hilo limekuwa likimuweka jirani zaidi na wananchi na kufanya apendwe.
kutokana na
hulka yake ya kuwa na wananchi karibu amekuwa akiweka kipaumbele hasa
wanapokuwa na changamoto mbalimbali zikiwepo za ugonjwa.
Kiongozi huyu
amekuwa akionesha upendo wake kwa watu wote bila ubaguzi.
Katika
kudhihirisha upendo alionao Septemba 8, 2026, Badar Sood alifika Kizimkazi Mkoa
wa Kusini Unguja, Zanzibar kumfariji Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dk. Samia Suluhu Hassan kufuatia kufiwa na Mume wake Marehemu Maalim Hafidh
Ameir Hassan, aliyefariki dunia katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena
Zanzibar wakati akipatiwa matibabu, Septemba 07, 2026.
Jambo hilo
siyo dogo kwani ni la kiimani zaidi na dini zote zimekuwa likihimiza.
Maisha ya Badar Sood yamekuwa kielelezo kwa
wana Tanga na Taifa kwani ni mtu mwenye hofu ya Mungu na asiye jikweza.
.......................
Habari hii imeandaliwa na Dotto Mwaibale Simu namba 0754362990.










No comments:
Post a Comment