Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Jesca Kishoa akizungumza na Wananchi wa Kata ya Ibaga, Wilaya ya Mkalama wakati alipokuwa katika ziara yake ya kikazi wilayani humo Aprili 21, 2024.
..........................................
MBUNGE wa Viti Maalum Mkoa wa Singida, Jesca David Kishoa Jumamosi amefanya ziara ya kikazi katika kata ya Ibaga, Wilaya ya Mkalama ambayo ilikuwa mahsusi ya kumuunga mkono Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri anayoifanya katika kuliongoza na kuliletea maendeleo Taifa letu. ambapo pia alitatua kero mbalimbali za wananchi kama ifuatavyo:
1. Kugawa Mitungi ya gesi ya kupikia Kwa kinamama wajasiriamali (Mama Lishe) 30.
2. Kugawa jezi za mpira Kwa timu 15 zinazotoka Kata ya Ibaga.
3. Ametembelea na kuchangia kiasi cha Tshs. 3,700,000/= ili kumalizia ujenzi wa zahanati ya Ibaga.
4. Ameviunga mkono vikundi 26 vya wanawake, wazee na vijana kwa kuviongezea akiba ya fedha kwenye shughuli zao.
5. Pia ametatua kero ya mgonjwa aliyepata ajali katika Kijiji Cha Ibaga na kesho mgonjwa huyo ataendelea na matibabu Hospitalini.
Aidha Mheshimiwa Mbunge amewahamasisha wananchi
kudumisha mshikamano na kumuunga mkono Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Wanawake wa Kata ya Ibaga wakiwa na majiko ya gas waliyopewa na mbunge huyo














No comments:
Post a Comment