.......................................
Na Mwandishi Wetu
Viongozi wa Serikali hususan mawaziri wametakiwa kuiga
uchapakazi wa Naibu Waziri Wizara ya Sayansi na Teknolojia, Mhe. Maryprisca
Winfred Mahundi.
Wito huo umetolewa na mmoja wa wananchi aliyekuwa na
changamoto ya binti yake aliyeomba namba ya NAPA kwa lengo la kupata mkopo wa
elimu ya juu, mtandao ukawa hauruhusu taarifa zake kufunguka alivyomsaidia
kutatua tatizo hilo kwa muda mfupi.
Mwananchi huyo ambaye ameomba kuhifadhiwa jina lake amesema jana
usiku aliwasiliana na waziri huyo na kumueleza changamoto yake ambapo
alimueleza kuwa atamfahamisha msaidizi wake atakayempigia simu mwananchi huyo leo
hii asubuhi (Agosti 23, 2025) ili afuatilie kujua tatizo liko wapi.
"Asante kwa taarifa na pole sana kwa changamoto hiyo,
ninawasiliana na msaidizi wangu, atafuatilia kujua tatizo lipo wapi halafu
mapema kesho asubuhi (Leo tarehe 23) atakupigia simu," mwananchi huyo
alimnukuu Waziri Mahundi.
Mwananchi huyo ameongeza kuwa mapema asubuhi alipigiwa simu
na mtu aliyejitambulisha kwa jina moja la Simon kwamba ni msaidizi wa Naibu
Waziri Maryprisca aliyempa taarifa za changamoto yake akaomba amweleze.
Amesema alipomfahamisha, alimuunganisha kwa Afisa wa NAPA
aliyemueleza changamoto yake.
"Nilimwambia kwamba tangu nilipoomba namba ya NAPA
mapema mwezi huu kila nilipofungua mtandao kujua kama ombi langu lilikubaliwa
nilijibiwa bado linashughulikiwa, nikakosa amani kwani siku zinaisha ambapo
tarehe 31 saa 6 usiku zoezi hilo linafungwa," mwananchi huyo alisema.
Aliongeza kuwa baada ya kumfahamisha hivyo na kumpa namba
yake ya simu na kuingia kwenye mfumo alibaini kilichosababisha hali hiyo
akakiweka sawa, muda huo huo mtandao ukafunguka na binti yake aliyemtaja kwa
jina moja la Diana akapata ujumbe wa hongera kwenye simu yake kuonesha amepata
barua ya kuombea mkopo kupitia NAPA.
"Nimefurahi sana bila waziri huyo kunisaidia kwa upendo
binti yangu angekosa fursa ya kupata mkopo wa elimu ya juu. mawaziri wengine
waige uchapakazi wake wa kuwasaidia wananchi, namuomba Rais Samia kutowaacha mawaziri
wa aina yake kwenye baraza lake la mawaziri baada ya uchaguzi mkuu, au kuwapa
nafasi sehemu nyingine ili waendelee kuwatumikia watanzania," alisema
mwananchi huyo huku akitabasamu.
Aidha, amemshukuru afisa wa NAPA aliyemtaja kwa jina moja la
Amani na msaidizi wa waziri jinsi walivyoishughulikia changamoto ya mwananchi huyu
kwa haraka.










No comments:
Post a Comment