DKT. ASHA- ROSE MIGIRO MWANAMKE WA KWANZA KUWA KATIBU MKUU CCM - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, August 23, 2025

DKT. ASHA- ROSE MIGIRO MWANAMKE WA KWANZA KUWA KATIBU MKUU CCM

Katibu Mkuu wa CCM Taifa, Dkt. Asha-Rose Migiro

................................................

Na Dotto Mwaibale, Dar es Salaam

Dkt. Asha-Rose Migiro ni mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), nafasi ambayo haijawahiu kushikwa na mwanamke yeyote tangu Tanzania ipate uhuru wake mwaka 1961.

Nafasi hiyo ya Dkt. Migiro imekuja kufuatia uteuzi uliofanywa na Kikao cha Halmashuri Kuu ya CCM (Taifa) chini ya Mwenyekiti wake na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Dkt. Migiro anashika nafasi hiyo ya juu katika chama hicho akimrithi Dkt. Emmanuel Nchimbi ambaye aliteuliwa kuwa mgombea mwenza wa Dkt. Samia wa nafasi ya urais kupitia chama hicho.

Pamoja na kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa CCM,Dkt. Migiro ana historia ya kipekee pia nchini kwani ni mwanamke wa kwanza kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa chini ya Katibu Mkuu wa umoja huo aliyestaafu Ban Ki-moon...SOMA ZAIDI

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad