Katika kijiji kimoja mkoani Arusha, aliishi kijana aitwaye Lameck.
Alikuwa kijana ambaye maisha yake yalijaa changamoto tangu utotoni.
Baada ya kumaliza masomo ya sekondari, hakupata ajira wala nafasi ya kuendelea na masomo ya juu kutokana na ukosefu wa fedha.
Kwa muda mrefu alikuwa akikaa tu nyumbani, akitegemea chakula na msaada kutoka kwa wazazi wake.
Hali hii ilisababisha watu wengi kumdharau.
Wazazi wake waliona kana kwamba hana msaada kwa familia, ndugu walimchukulia kama mzigo, na hata marafiki zake wa utotoni walimkejeli wakisema, “Lameck ni mtu wa kukaa tu nyumbani, hana lolote.”
Maneno hayo yalimuumiza sana moyoni, lakini hakuwa na njia nyingine zaidi ya kuvumilia...SOMA ZAIDI










No comments:
Post a Comment