Kuwa landlord sikuwa nimepanga maishani mwangu. Baada ya miaka mingi ya kujinyima na kufanya kazi kwa bidii, nilifanikiwa kujenga nyumba ndogo ya kupanga. Haikuwa kubwa sana, lakini ilikuwa chanzo kizuri cha mapato ambacho kilikuwa kinanisaidia kulipa bills za nyumbani na kusaidia familia yangu.
Mwanzoni mambo yalikuwa yanaenda vizuri. Wapangaji wangu wengi walikuwa waelewa. Walikuwa wakilipa kodi kwa wakati, na kulikuwa na amani nzuri kwenye nyumba ile. Kwa kweli nilikuwa najivunia hatua niliyokuwa nimefikia.










No comments:
Post a Comment