𝐃𝐊𝐓. 𝐌𝐖𝐈𝐆𝐔𝐋𝐔 𝐀𝐑𝐄𝐉𝐄𝐀 𝐍𝐂𝐇𝐈𝐍𝐈 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐎𝐊𝐄𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐟𝐃𝐁, 𝐂𝐎𝐍𝐆𝐎 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Thursday, May 28, 2026

𝐃𝐊𝐓. 𝐌𝐖𝐈𝐆𝐔𝐋𝐔 𝐀𝐑𝐄𝐉𝐄𝐀 𝐍𝐂𝐇𝐈𝐍𝐈 𝐀𝐊𝐈𝐓𝐎𝐊𝐄𝐀 𝐌𝐊𝐔𝐓𝐀𝐍𝐎 𝐖𝐀 𝐀𝐟𝐃𝐁, 𝐂𝐎𝐍𝐆𝐎

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba amerejea nchini Tanzania akitokea jijini Brazzaville, Jamhuri ya Kongo alikomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 61 wa Mwaka wa Bodi ya Magavana wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB).

Dkt. Mwigulu aliagwa na Meya wa Jiji la Brazzaville, Dieudonné Bantsimba katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Maya Maya, Brazzaville Mei 27, 2026.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad