MKUTANO MKUBWA WA INJILI KUTIKISA DAR ES SALAAM - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Saturday, June 13, 2026

MKUTANO MKUBWA WA INJILI KUTIKISA DAR ES SALAAM

Wagonjwa, wenye shida kuombewa bure


 Mchungaji Dr. Lucas Dobogo

...............................

Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Kigogo Kati Jijini Dar es Salaam limeandaa mkutano mkubwa wa injili wa siku saba za wokovu, uponyaji naa kufunguliwa.

Akizungumza na waandishi wa habari Mchungaji mwenyeji wa mkutano huo, Dr. Lucas Dobogo alisema mkutano huo utaanza Juni 22, 2026 na utafikia tamati Juni 28, 2026.

“Mkutano huo utafanyika Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT), Kigogo Kati Jijini Dar es Salaam kuanzia Saa 9 alasiri  kila siku watu wote wanakaribishwa,” alisema Mchungaji Dobogo.

Alisema katika mkutano huo Kwaya ya Victory ambayo itakuwa mwenyeji na Kwaya ya Palanjo Family kutoka Arusha zitahudumu.

Aidha, Mchungaji Dobogo alisema kwenye mkutano huo wagonjwa, watu wenye shida mbalimbali wataombewa bure na amewataja Wachungaji watakao hubiri kuwa ni Joseph Ndaki, Keneth Mazengo na Dr. Lucas Dobogo.

Kwa mawasiliano zaidi kuhusu mkutano huo unaweza kupiga namba 0658972055 na 0686815230.

......................

Habari hii imeandikwa na Dotto Mwaibale Simu namba 0754-362990

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad