𝐓𝐔𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐆𝐄𝐑𝐄𝐙𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐈𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐀𝐊𝐈𝐒𝐈 𝐌𝐀𝐆𝐄𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐉𝐈𝐍𝐀𝐈 𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀 - SINGIDANIBLOG

Habari za Hivi Punde

Post Top Ad

Tuesday, May 26, 2026

𝐓𝐔𝐙𝐎 𝐘𝐀 𝐌𝐀𝐆𝐄𝐑𝐄𝐙𝐀 𝐊𝐖𝐀 𝐑𝐀𝐈𝐒 𝐒𝐀𝐌𝐈𝐀 𝐈𝐋𝐈𝐕𝐘𝐎𝐀𝐊𝐈𝐒𝐈 𝐌𝐀𝐆𝐄𝐔𝐙𝐈 𝐘𝐀 𝐌𝐅𝐔𝐌𝐎 𝐖𝐀 𝐇𝐀𝐊𝐈 𝐉𝐈𝐍𝐀𝐈 𝐓𝐀𝐍𝐙𝐀𝐍𝐈𝐀


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo ya kuwa Kinara wa Dhana ya Urekebishaji wa Wafungwa Magerezani kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Paschal Katambi pamoja na Kamishna Jenerali wa Magereza Jeremia Yoram Katungu kwenye hafla ya hafla ya kuhitimisha Mafunzo ya Uongozi Ngazi ya Juu Kozi namba 28 na Uongozi Daraja la Pili Kozi namba 48 ya mwaka 2025/2026 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCT) Ukonga Jijini Dar es Salaam Mei 9, 2026.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akionesha tuzo hiyo.

.......................................... 

KWA mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Jeshi la Magereza Tanzania, mkuu wa nchi, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan ametunukiwa Tuzo Maalumu ya Kinara wa Dhana ya Urekebishaji wa Wafungwa Magerezani (Champion of Prisoner Rehabilitation Concept Award) hatua inayotajwa kuwa ishara ya mageuzi makubwa ya kifalsafa, kiutendaji na kimaendeleo ndani ya mfumo wa haki jinai nchini.

Tuzo hiyo aliyokabidhiwa Rais Samia, Mei 9, 2026 katika Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania haionekani tu kama pongezi kwa uongozi wa Serikali, bali kama alama ya mabadiliko ya kihistoria yanayoibadilisha falsafa ya magereza kutoka mfumo wa adhabu kwenda mfumo wa urekebishaji, elimu na maendeleo ya binadamu.

Mageuzi hayo yanasimamiwa kwa karibu na Mkuu wa Jeshi la Magereza nchini, CGP Jeremiah Yoram Katungu, ambaye chini ya uongozi wake jeshi hilo limeendelea kufanya maboresho makubwa ya kiutendaji, matumizi ya teknolojia na utoaji wa mafunzo ya kisasa ya urekebishaji.

KUENDELEA  KUSOMA MAKALA  HII 

...BOFYA HAPA...

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad